ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, May 19, 2011

KAMA NI VIPAJI, PENYEWE SINDIYO HAPA!!

Taifa stars ya baadae.
Mwishoni mwa wiki nilipata fursa ya kutembelea viwanja vya shule ya msingi Igoma wilaya ya Ilemela jijini Mwanza, askwambie mtu nilikutana na watoto wadogo wanasukuma kandanda balaa, wakicheza mpira wa makaratasi aka cha ndimu huku wakizingatia sheria kadhaa za soka(ingawa siyo zote)


Mashambulizi yakiendelea kwa nyuma beki akipiga mahesabu ya kuuondosha katika hatari..

Mshambuliaji mara baada ya kuwatoka walinzi hapa akielekea langoni kuzifumania nyavu.

Kama ni suala la nidhamu na utii upo ...Wakubwa wakipita watoto hawa wana utaratibu wa kusimamisha mchezo (yaani pale pale ulipo) kisha wakisha pita mchezo unaendelea kama kawa...

Mwanza kuna timu nyingi sana za watoto (U14) tena zenye vipaji na walimu wazuri wa kujitolea wa soka, ukitembelea vituo hivyo matatizo ni yale yale 'uwezeshwaji'

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.