ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, April 22, 2011

TUNAWATAKIA IJUMAA KUU NJEMA

Leo ni Ijumaa Kuu, siku ambayo Bwana wetu Yesu Kristo alikufa msalabani kwa ajili yetu.Na haya ndiyo maandalizi: Mbuzi aliyenona kwaajili ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka.

WAKITOKA KANISANI LEO IBADA YA IJUMAA KUU.
Sio kwenda kanisani au kuimba mapambio tu kwamba ndiko kutakompatia mwanadamu uzima wa milele bali matendo. Japo ni muhimu kujumuika na waumimni wenzetu makanisani,la muhimu zaidi ni kuishi kwa mfano wa Bwana Yesu ambaye licha ya upendo wake usiomithilika alikuwa tayari kufa msalabani kwa dhambi zetu ili atuletee ukombozi.

Wakati tovuti hii inakutakia wewe msomaji mpenda Ijumaa Kuu njema,siku hii inaweza kuadhimishwa ipasavyo kwa kutafakari kuhusu upendo wa Bwana,kujitoa kwake kwa ajili yetu na upendo kwa ujumla. Kama humpendi jirani yako unayemwona kila siku utakuwa mnafiki kudai unampenda Bwana mbaye hujawahi kumwona. Yesu ni upendo na amani.

"NAWATAKIA IJUMAA KUU NJEMA"
@G.Sengo

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.