ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, April 12, 2011

MIAKA 26 KIFO CHA SOKOINE: HAKUNA KIONGOZI WA KUVAA VIATU VYAKE.

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa vipindi viwili (3 Februari 1977 na 7 Novemba 1980) na(24 Februari 1983 to 12 Aprili 1984), Hayati Edward Moringe Sokoine, anakumbukwa leo. SOKOINE alifariki kwa ajali ya gari huko Dakawa, Morogoro tarehe 12 Aprili 1984 na sasa yapata miaka 26 tangu tukio hilo lililozua simanzi kutokea. Kutakuwa na misa ya kumbukumbu ya kifo chake katika kanisa la Mt Joseph jijini leo jioni iliyoandaliwa na familia ya kiongozi huyo wa zamani aliye heshimika sana nchini.

HIVI MAJUZI:-
Serikali ya Mkoa wa Morogoro kwa kushirikian na Wilaya ya Mvomero, tayari zimetenga Sh bilioni 12 kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya juu itakayokuwa na Kidato cha Tano na Sita eneo la Kijiji cha Wami Ruhindo, alipofia aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Moringe Sokoine.

Shule hiyo imepewa jina la Sokoine Memorial High School, ambapo ujenzi wa awamu ya kwanza iliyotengewa kiasi cha sh bilioni tatu unatarajia kuanza Mei, 2011 na kukamilishwa Desemba 2011 na wanafunzi wa kwanza wa kidato cha tano wanatarajia kuanza mapema Februari 2012.


SWALI:-
Je! VIONGOZI WETU WANAENZI VIPI MAWAZO YAKE KATIKA KUSIMAMIA RASLIMALI ZA TAIFA LETU?

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.