ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, March 27, 2011

SHANGWE ZALIPUKA WAKATI 20% AKING'ARA TUZO ZA KILIMANJARO 2011: MAPINDUZI YAONEKANA

Tuzo zenye hadhi ya juu Afrika Mashariki zenye jina 'Tanzania Kilimanjaro music Award' hatimaye zimefanyika ndani ya Diamond jubilee jijini Dar es salaam huku msanii wa muziki wa Bongo Fleva 20%aking'ara kwa kuondoka na tuzo 5 ndani ya vipengere tofauti. Producer Man Walter alipokea tuzo zote kwa niaba ya 20%

20% AMENYAKUWA TU HIZI:
Msanii bora wa kiume,
Mwimbaji bora wa kiume,
Wimbo bora wa mwaka- Tamaa mbaya.
Mtunzi bora wa nyimbo,
Wimbo bora wa Afro pop- Tamaa mbaya.


Barnaba toka THT hakika alistahili kuitwaa tuzo hii Wimbo bora wa zook/rhumba kupitia wimbo Nabembelezwa: Naaaam - ilimilikishwa huku akishangiliwa na hadhira iliyo kuwa eneo la tukio.

Mwanamuziki mkongwe kutoka Msondo ngoma music band Said Mabela akitoa zake shukurani mara baada ya kutunukiwa Tuzo ya Hall Of Fame mie naiita Tuzo ya Uvumilivu, kwa ufupi mcharazaji huyu wa gitaa la solo hajawahi hama bendi hiyo tangu ajiunge nayo, yaani bendi inabadili majina yeye yupo tuu mpaka leo.

Kwake binafsi wakati akizungumza mara baada ya kupokea tuzo ya Wimbo bora wa asili wa Tanzania, Mpoki wa Orijino Komedi alisema "Kwangu mimi kupokea tuzo hii ni maajabu ndani ya maisha yangu, kwani kupata tuzo hii kwangu mie ni sawa na mwanamke asiye na mimba kuzaa..."

Joe Makini akifanya mahojiano na Swahiba Antonio Nugaz wa clouds Tv mara tu baada ya kuitwaa kwa mara nyingine tena tuzo ya Msanii bora wa Hip Hop wa Mwaka.

Ni katika kuenzi kazi za wakongwe katika burudani usiku wa 'red kapeti' Wasanii maarufu Diamond (mbele), Ali Kiba (shoto) na Banana Zorro (kulia) wakiimba wimbo 'Wanaume tumeumbwa mateso' wa Msondo nakuutia nakshi ambazo kwa kila aliye na jicho alisema naaam!
Usiku huu hakika ulikuwa mzuri sana kwa bidada huyu mdogo aliye na sauti ya kumtoa nyoka pangoni, LINAH alinyakuwa tuzo mbili: Msanii mpya anayechipukia na Mwimbaji Bora wa kike.

Ben Paul alitoka kidedea Wimbo bora wa RnB - Nikikupata.

Pichani Shabiki mteule wa Lady Jaydee akipokea tuzo kwa niaba yake ikiwa ni katika tuzo ya Msanii bora wa kike then tuzo ya pili wimbo bora wa Afrika Mashariki akishirikishwa na Kidumu.

Best Rapper of The Year (Band) Khalid Chokoraa na maswahiba wake Mapacha watatu.

Kaseja akimtunukisha Mzee Yusuph tuzo ya Wimbo bora wa taarab - My Valentine.

Mie na President wa Tanzania House of Talents ambaye vilevile ni mmoja wa wakuu wa bodi ya Clouds Media Group Mr Ruge Mutahaba.

'Shika ushikapo' toka kwao Mapacha watatu ft Mzee Yusuph ni wimbo ulionyakuwa tuzo ya Wimbo bora wa kiswahili.

Much Respect Kutoka kushoto: Bonta, J moo, G.sengo, Joe Makini na Niki wa Pili.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.