ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Sunday, February 27, 2011

MAAFANDE WA MWANZA WAUAGA MWAKA NA KUUKARIBISHA 2011 NA BONGE LA SHEREHE LILILOFANYIKA KATIKA MOJA YA FUKWE ZA ZIWA VICTORIA

Polisi Jazz aka Wana Orch Vangavanga toka jijini Dar es salaam ndiyo walikuwa wamwaga burudani.

'Tukumbuke na kuzingatia viapo tulivyoapa' Kamanda S. Sirro ktk nasaha.

Makaribisho hayo ya mwaka mpya 2011 pia yalikwenda sambamba na utoaji wa Tunzo za shukurani kwa wadau walioshiriki kwa karibu katika kulisaidia jeshi la polisi Mwanza Pichani MNEC Mr Gachuma akipokea yake toka kwa mgeni rsmi mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro.

Mambo ya maakuli yalikuwa si polepole 'full drafti'

Maafandez dadaz nao waling'ara!

Mc wa sherehe hiyo aliyeichangamsha ile kisawasawa Prince Baina Kamukulu akiikaribisha meza kuu kufungua muziki.

Flowers wakisebeneka na ile mipigo ya **Prakatatu-tantu-tantu, Prakatatu-tantu-tantu...***

Wau! maafisaa wa sheria nao Ndani'

Meza makini ya watu makini.

"Habari zenyu! mnakunywaa au mnatania, vipi vinywaji vimeishaa, tu-mi-ke-ni leo siku yetu" Kamanda Sirro alipita meza baada ya meza akikagua huduma kama zinasomeka.

Hapa ilikuwa ni kama ka-ligi hivi ka kushindana kucheza baina ya Kamanda Sirro na wafanyabiashara wawili maarufu jijini Mwanza Mr.Kihelya na Mr.Kitana. Basi wacha watu wajitume kukumbushia za enzi na enzi Dah!

ChiaaaaazZZz!

"Hebu njooni Tupige moja ya ukumbusho"

Ewaaa!!
Sherehe hii ya kufana ya Jeshi la polisi Mwanza kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011 ilifanyika jana jumamosi katika fukwe za Yatch Club ikiwa na lengo la kukumbushana sera kuu ya umoja kwa jeshi hilo sambamba na umuhimu wa kushirikiana na wananchi katika kudhibiti na kuzuia uhalifu nchini.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.