ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, February 2, 2011

NANI KAKWAMBIA MWAKA MPYA ULIKARIBISHWA KWA AMANI NA UTULIVU? ALAMBWA RISASI NA POLISI WAKATI AKIUKARIBISHA MWAKA.

Usiku wa kuukaribisha mwaka mpya 2011 kwa wengi huwa ni wa furaha, lakini kwa dada huyu kwake ulimwendea kombo kwa kukutana na balaa la kupata kilema cha maisha mara baada ya kushambuliwa kwa kupigwa risasi mguu wake wa kulia na mtu inayesemekana kuwa ni askari wa jeshi la polisi ambaye mpaka sasa jina lake halijatajwa.Usiku wa saa sita na dakika zake, dada Lilian James akiwa na mpenzi wake wakielekea nyumbani kwao Mabatini, wakitokea stand ya zamani ya mabasi Mwanza walipofika eneo la 'Kileluu Mabatini' wakakutana na kundi kubwa la watu wakikimbia ambao walikuwa wakitawanywa na polisi kutokana na vurugu zilitokea usiku huo ambazo zimekuwa kama jadi kwa kila nyakati za kuukaribisha mwaka kwa baadhi ya watu kufanya uharibifu wa kuvunja vioo vya baadhi ya magari na kupora mali hasa eneo hilo la barabara ya mabatini-igoma. Wasielewe kinachoendelea na kujitenga na wakimbiao, mlio wa risasi ukasikika-'TPBUUU!!' Mwanaume akatimua mbio, mwanamke akashindwa kukimbia hata kusogeza mguu kwani risasi moja ilikuwa tayari imetandika mguu wake wa kulia.

Kesi bado iko polisi ikizungushwa isijulikane nini mstakabari wake na hata maafisa wa jeshi la polisi Mwanza hawajazungumza lolote kwa kilichotokea zaidi ya kupinga kwa kusema kuwa haikuwa risasi bali ni bomu la machozi.

Na kwa mujibu wa mwanaume wa Lilian James amesema kuwa kulipo pambazuka walikwenda polisi na vithibitisho vya maganda ya risasi ambavyo walipigwa mkwara na askari kisha kunyang'anywa kwa nguvu.


INAENDELEA......

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.