ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, January 26, 2011

SIKU ALIPOSIMIKWA ASKOFU MKUU JIMBO KUU KATOLIKI LA MWANZA MHASHAMU JUDE THADDAEUS RUWA'ICHI.

Ni siku ya jumapili ya tarehe 9 mwezi january 2011, katika kanisa katoliki Kawekamo jijini Mwanza, ndipo shughuli rasmi ya kumsimika Askofu Mkuu mpya jimbo la Mwanza, mhashamu Jude Thaddaeus Ruwa'Ichi ilipochukuwa nafasi.

KADINARY PENGO (KUSHOTO) NA RUWA'INCHI.
Tukio hili la usimikwaji limekuja mara baada ya Taarifa zilizotoka mwishoni mwa mwaka jana kutolewa kutoka Ubalozi wa Vatican nchini kwenda kwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), ikielezea uteuzi huo na kufafanua kuwa Askofu Mkuu Ruwa’ichi anapaswa kwenda kuziba nafasi ya aliyekuwa Askofu wa jimbo hilo, Anthony Mayalla aliyefariki dunia Agosti 19, mwaka juzi.

Askofu Ruwa’ichi ambaye pia ndiye Rais wa TEC amekuwa mwanashirika wa watawa wa Mtakatifu Fransisco kwa kipindi kirefu.

Wageni waalikwa na wadau wa kanisa.

Wageni mbalimbali toka serikalini nao walipata mwaliko kuhudhuria sherehe hizo. Kutoka kulia Waziri Stephen Wasira, mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbas Kandoro, mama, mtoto, Mbunge wa Ilemela Mh.Hainnes Samson na Mh.Wenje mbunge wilaya ya Nyamagana.

Sifa na shukurani kupitia nyimbo.

Askofu Ruwa’ichi ambaye pia ni Rais wa TEC, alizaliwa Januari 30, 1954 katika Wilaya ya Moshi, Kilimanjaro na alipata Daraja la Upadri Novemba 25, 1981 kabla ya kuteuliwa kuwa Askofu wa Jimbo la Mbulu, Februari 9, 1999.

Kamati ya itifaki, mapokezi na usalama wa viongozi wa serikali ilisimamiwa barabara na wadau hawa:- kutoka kushoto Joseph Mlinzi ambaye ni afisa uhusiano wa jiji na Patrick Karangwa huyu ni mchumi wa jiji.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.