ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Tuesday, January 11, 2011

KWETU KWA WAZAZI.

Ilikuwa siku ya jumamosi ya tarehe 8.jan.2011 kaka yangu aliwasiliana nami kwamba anaelekea Mwanza na familia yake kwa likizo fupi na kusema kuwa kabla ya kufika Rock City atapitia kijijini kwetu pale Malampaka Shinyanga kwaajili ya misa fupi kwenye kaburi la marehemu baba yetu George Sospeter Sengo aliyeaga dunia mnamo mwaka 1988. Pichani mbele ni Aliyerithi jina la mzee ni mtoto George (wa bro Adam Sengo) mbele ya kaburi la babu yake. Nami ilinipasa kujumuika nao ingawa kuna misa kuu ya kifamilia tunayotegemea kuifanya siku za baadaye.

Japo kwa uchache familia yetu.

Brother Adam mbele ya kaburi la babu yetu Mzee Sospeter, kaburi lililopo hatua chache toka kaburi la marehemu baba.

Watoto wanapenda sana kujifunza kwa kuuliza maswali tena mengi ya kudadisi, hili nililiona kwa mtoto huyu wa braza ambaye nae aliomba kupiga picha ya kumbukumbu.

Hazina za kwetu milima ya mawe.

Wakati wa umiliki wa eneo hili kupitia Tajiri mmoja aliyekuwa mwekezaji wa magari yaliyokuwa na chata 'REHEMA YA MUNGU' namzungumzia Paul Ng'wani, Kituo hiki cha mafuta kilikuwa kinang'aa kisawasawa yaani hapa ndiyo penyewe, town centre babaake!.

Aya-ya-yaaa Fagia sana kiwanja hapo mbele... 'Home sweet home' nyumbani kwa Mzee Kaseko.

George na Nduguye mpya katika pozi.

Hiki ni moja kati ya kitaa kilicho shiriki kunikuza (just for three years). "Kiukweli kama neema imepotea hivi tofauti" nakumbuka Enzi hizo nyumba zilikuwa smati na hata kama za udongo zilinakshiwa na chokaa huku watu wakishindana kupanda maua mbele ya nyumba yaani full green. Lakini sasa MMMMh!

Tupe maoni yako

1 comments:

  1. mji gani huu Albert,safi sana kwa kukumbuka nyumbani,na pole pia kwa kumpoteza mzee

    ReplyDelete

Note: Only a member of this blog may post a comment.