ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Saturday, May 8, 2010

SEMINA YA BIASHARA YAFANYIKA MWANZA LEO.

SEMINA KUBWA YA BIASHARA INAYOHUSISHA EAST AFRICA NZIMA IMEFANYIKA LEO JIJINI MWANZA KATIKA UKUMBI WA BOT HALL CAPRIPOINT.

WATAALAM WA BIASHARA TOKA FOREVER LIVING PRODUCT NDIYO WALIOKUWA WATOA MADA.

WANASEMINA WAKIFUATILIA MAMBO KWA UMAKINI AMBAPO HUMU NDIMO CHIMBUKO LA FURSA INAYOAMSHA HARI YAKUFUFUA NDOTO ZA KILA MPENDA MAENDELEO DUNIANI.

TANZANIA OYEEE!


KUPITIA MKUTANO MKUBWA WA DUNIA WA UCHUMI ULIOFANYIKA NA KUMALIZIKA LEO JIJINI DAR ES SALAAM HAKIKA TAIFA LETU LIMEFUNGUA UKURASA MPYA WA FURSA YA KIUCHUMI.

MKUTANO HUU WA 20 MAHUSUSI KWA BARA LA AFRIKA, ULIRATIBIWA NA JUKWAA LA UCHUMI DUNIANI LENYE MAKAO MAKUU HUKO GENEVA USWISI.

MKUTANO UMEFUNGUA MILANGO YA KIUCHUMI KWA TAIFA LETU, KUTOKANA NA UKWELI KWAMBA SASA TUMEINGIAKTK RAMANI YA UCHUMI WA DUNIA KWA KUFANYIKA MKUTANO HUU HAPA NCHINI KWANI KWA KIPINDI KIREFU MIKUTANO MINGI IMEKUWA IKIFANYIKA AFRIKA YA KUSINI KUTOKANA NA NCHI HIYO KUWA NA MIUNDOMBINU BORA ZAIDI YA KUHUDUMIA WAGENI WENGI KWA PAMOJA, KIGEZO AMBACHO TANZANIA IMEKITIMIZA HATIMAYE IKAWA MWENYEJI WA MKUTANO HUO ULOMALIZIKA KWA UFANISI.

ZAIDI YA WAGENI 1000 KUTOKA NCHI 85 WAKIWAMO WAKUU WA NCHI 11 WAMESHIRIKI MKUTANO HUU, DHAHIRI HALI IKIONESHA KUWA KUTOKANA NA MKUTANO HUU MIKUTANO MINGINE YA KIMATAIFA ITAKUWA IKIFANYIKA HAPA NCHINI KWANI WAGENI WANASIFA YETU NA UZOEFU WETU KTK KUFANIKISHA MIKUTANO MIKUBWA KAMA HUU ULIOISHA.

LENGO LA MKUTANO PAMOJA NA KUJADILI NA KUBADILISHANA UZOEFU WA KUJENGA UCHUMI NA KUIMARISHA UHUSIANO WA KATI YA MATAIFA YENYE UCHUMI MKUBWA NA YALE YA AFRIKA MAARUFU KAMA SOUTH - SOUTH CO - OP - ERATION.

Thursday, May 6, 2010

KAUTARATIBU KAPYA.

IMEKUWA SUALA LA KAWAIDA KUZIDISHIWA BILL NA WAHUDUMU KTK ILE TOTAL AU KUUZIWA VINYWAJI NA CHAKULA KWA BEI TOFAUTI NA ILE HALALI ILIYOPANGWA NA BAA/HOTEL HUSIKA. SASA MWANAWANE ILI TUSIENDELEE KUPIGWAAAA, KUNA HAKA KAUTARATIBU KAMEFANYIKA PALE ROYAL PUB (BANGO LENYE BEI HALALI), KUWEKA MENU KILA MEZA BAJETI KIBONGOBONGO HAIRUHUSU HEBU TUWASHAURI NA WADAU WENGINE WAIGE MFANO HUU. AU SIYO
UKIPIGWA BASI UMETAKA MWENYEWE!

MWANZA LEO..


HALI YA LEO MAOFISINI NA SHUGHULINI MWENDO NI MASWETA NA MAKOTI ANGANI KITU CHA MWAMVULI.

BGML YATOA MSAADA WA SHILINGI MILIONI 50 KWA WAHANGA WA MAFURIKO.


PICHANI Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Meja mstaafu Bahati Matala, wa pili kutoka kulia mstari wa mbele akipeana mkono na Meneja Mahusiano na Serikali wa African Barrick Gold, Philbert Rweyemamu.

HABARI KAMILI:-Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu umetoa msaada wa shilingi milioni 50 kwa waathirika wa mafuriko wilayani Bukombe na pia kusaidia wilaya hiyo katika kuanzisha Mfuko wa Maafa.
Akikabidhi hudi ya fedha hizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Meja mstaafu Bahati Matala, Meneja Mahusiano na Serikali wa African Barrick Gold, Philbert Rweyemamu, amesema kampuni imeguswa na maafa hayo ya mafuriko katika wilaya ya Bukombe.
“African Barrick Gold haiko nchini kwa ajili ya kuchimba madini pekee, bali pia kuisaidia jamii katika shughuli za maendeleo na kubwa zaidi wakati wa matatizo pia,” alisema Rweyemamu.
Rweyemamu alisema ABG kama mwekezaji katika sekta ya madini nchini Tanzania, itaendelea kufanya kazi na serikali katika kuhakikisha kuna maendeleo endelevu katika jamii inayozunguka migodi yake na kutoa msaada wa aina yoyote kwa wananchi.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya aliipongeza BGML kwa kuitikia haraka wito wa kutoa msaada na kuongeza kuwa fedha hizo zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.
Alifafanua kwamba, msaada huo utazilenga kaya 421 katika vijiji vya Lelembela na Kabanga kata ya Ikunguigazi ambazo nyumba zao zilibomolewa na mafuriko kutokana na mvua kubwa zilizonyesha Aprili 2 2010.
Kadhalika mvua hizo pia zilisababisha vifo vya watu watatu na daraja lililopo kati ya Runzewe na Ushirombo katika barabara kuu iendayo Rwanda na Burundi kusombwa na maji, hali iliyosababisha barabara hiyo kufungwa kwa siku mbili.
Jumla ya hekari 4,700 za mazao pia ziliharibiwa na mvua hizo.
Msaada huo wa fedha utatumika kununulia mahitaji muhimu kwa wananchi ikiwa ni pamoja na madawa, chakula, mahema na vitanda.

Wednesday, May 5, 2010

MWALONI LEO.

LEO NA TULIANGALIE SOKO LA MWALONI KIRUMBA JIJINI MWANZA MAARUFU KWA BIASHARA YA DAGAA, NDIZI,MAFUTA, MAZAO MBALIMBALI YA CHAKULA NA BIDHAA NYINGINEZO. KIUNGANISHI KWA BIASHARA NA VISIWA VILIVYOKO NDANI YA ZIWA VICTORIA.

BIASHARA HUFANYIKA NDANI NA NJE YA NCHI. MF. CONGO, KENYA,,,,,

MITUMBWI YA WAVUVI WALETA MAZAO MBALIMBALI TOKA VISIWANI.

DAGAA HULETWA NDANI YA MAGUNIA ZIKIWA ZIMEKAUSHWA, MADALALI HUKABIDHIWA KISHA ....

BIASHARA MOJA HUSUKUMA BIASHARA NYINGINE.

DAGAA HUTOKA VISIWA VYA UKEREWE, KOME, UKARA,MAJITA, GOZBA, BUKOBA NA NK.

MZIGO ULIO TAYARI KUSAFIRISHWA.

MADALALI KAZINI.

BIASHARA YA NDIZI INA NAFASI KUBWA NDANI YA SOKO LA MWALONI.

HAKITUPWI KITU HAPA! WAKATI MAGANDA HUWA LISHE KWA MIFUGO MPANGO MZIMA KWA ZILE NDIZI AMBAZO HUROJEKA SANA BAADA YA KUIVA HUMENYWA NA KUHIFADHIWA KWENYE NDOO NA KUUZWA KWA WATENGENEZAJI WA POMBE ZILEEEEE.

NDIZI HUIFADHIWA NAMNA HII ZISIPATE KUATHIRIWA NA JUA.

Tuesday, May 4, 2010

SAFARI HII WATU WATAKULA MCHELE.

SAFARI HII KANDA YA ZIWA ZAO LA MPUNGA LIMEKUBALI HASWAAA KUTOKANA NA MVUA NYINGI ZILIZONYESHA PAMOJA NA WAKULIMA KUANDAA NA KUPANDA MAPEMA.. INGAWA WENGI WALIPANDA KWA SHAKASHAKA! (msemo wa njogopa).

ENEO LA MASHINENI, MABATINI JIJINI MWANZA, MPUNGA UMESHEHENI HATA NJE YA VIWANDA. pichani moja ya kibanda cha kusaga na kukoboa nafaka..

MIZANI ZITUMIKAZO KIUKWELI ZINAUBORA, HAZIPUNJI KWANI MARA BAADA YA MANUNUZI NA KUFIKA KARIBU NA HOME NILIJARIBU KWENDA KWA MWENYE DUKA JIRANI NINAYE MFAHAMU NA KUUPIMA TENA MZIGO. KITU KIKASOMA SAFIIII!

BEI KWA SASA 800, 780, 750.

MCHELE SWAFI NAMI NIKAJICHUKULIA KILO KADHAA...

KWEA PIPA 3 YAPATA WENGINE MWANZA .

WADAU WA HABARI, WASHINDI NA WADAU WA NYANZA WAKIJICHANGANYA KWA YALIYOMO.

MSHINDI WA LUNINGA PILLY SAID KATO KUTOKA SHINYANGA MJINI, AKIPOKEA ZAWADI YAKE ALOJISHINDIA.

KULIA ATHUMANI SAID TOKA NYEGEZI MWANZA AKIZAWADIKA!

ZAWADI YA TIKETI KWENDA BONDENI SAFARI HII IMEKWENDA SHINYANGA KWAKE LEWIS MAJALA. MPAKA SASA KWA KANDA YA ZIWA TIKETI 10 ZIMETOKA, LUNINGA 3, NA MIZAWADI MINGINE KIBAO. WANYWAJI WAMESHAURIWA KUWA MAKINI KUANGALIA VIZIBO KABLA YA KUVITUPA.

HEPI BORZDAY DJ VENTURE!!


MLUME NDAGO LONG TIME KWENYE GAME, UMRI? MWALIMU WA FANI SASA. MWENYEZI MUNGU AKULINDE AZIDI KUWEKA MIKONO KATIKA KAZI YAKO, AKUONGEZEE HEKIMA NA UJUZI KADRI UNAVYO ISHI.... SAFI! HAPPY BORZDEY BROO.

Monday, May 3, 2010

WAJANJA WAZAMANI MPO?


HIVI UNAKUMBUKA YU AU YOLANDA AU PART 1 NA 2? WAJANJA WALIKUWA WANATUMIA