ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, December 9, 2010

SUSTAINET WAZINDUA VITABU VYA MBINU ZA KILIMO ENDELEVU.

Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mh. Serenge Mrenge akizindua vitabu vya mbinu sahihi za kilimo vya shirika lisilo la kiserikali la SUSTAINET hii ni mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa mwaka wa shirika hilo, uliofanyika Lakairo hotel Kirumba jijini Mwanza, nchini Tanzania. Katikati ni katibu mkuu mtendaji wa mradi huo Tom Apina akifuatilia tukio hilo kwa umakini.

VITABU VYA ELIMU JUU YA MBINU SAHIHI ZA KILIMO.
Mradi wa SUSTAINET umefanikiwa kujumuishwa kama sehemu ya mtandao wa UN kupitia shirika lake la chakula na kilimo - FAO umejikita zaidi katika kutoa elimu kwa wakulima wadogo na kushirikiana nao katika kuwaelekeza mbinu sahihi za kuanzisha miradi waweze kujikwamua kutoka katika lindi la umaskini kupitia kilimo chenye manufaa (kilimo cha biashara).

Katika mkutano huo wa mwaka Mada mbalimbali ziliwasilishwa na kujadiliwa na hatimaye maazimio ya mkutano yakawa ni pamoja na shirika hilo kujipanua zaidi kuhakikisha kuwa kila mkulima ananufaika na elimu wanayoitoa.

Mh. Serenge akikabidhiwa seti nzima ya vitabu vya KILIMO toka kwa Edith Omamo ambaye ni mratibu wa Mradi huo wa shirika lisilo la kiserikali la SUSTAINET unaodhaminiwa na watu wa Ujerumani wenye mtandao wa kiushirika kwa vikundi vya watu binafsi kwa nchi za afrika mashariki za Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda na Burundi.

Mkuu wa wilaya ya Ilemela akiangusha sahihi kwenye moja ya vitabu vya kilimo vilivyozinduliwa.

BOARD MEMBER NA MKUU WA WILAYA.
Traditional practices can be improved and combined with alternative ecological forms of land use, resulting in comprehensive systems for sustainable agriculture. A wealth of experience drawn from every continent confirms that these approaches have great potential, which is still significantly under-exploited. But before these successful approaches can be disseminated on a massive scale, numerous obstacles have to be overcome. Generally the potential users of sustainable agriculture do not have enough access to the information they need. An equally common problem is that political, social and economic structures in a country can inhibit the implementation of such approaches. Under the auspices of its National Strategy for Sustainable Development, the German federal government supports the SUSTAINET project, which aims to overcome these obstacles.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.