ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 17, 2010

MAELFU WAJITOKEZA MAZISHI YA DR. REMMY.

Hatimaye mwili wa gwiji wa muziki wa dansi nchini Ramazan Mtoro Ongalla maarufu kama Dr. Remmy Ongalla umezikwa jana katika makaburi ya sinza, Dar es salaam ambapo mamia ya wakazi walihudhuria mazishi hayo. Kabla ya kuzikwa mwili wa marehemu uliagwa katika viwanja vya Biafra vilivyopo Kinondoni, jijini Dar.
Mamia ya waombolezaji walilazimika kuvumilia adha ya kukanyagana wakati kila mhudhuliaji akijaribu kupata nafasi ya kumuaga mwanamuziki huyo aliyeacha watoto sita.


Waziri wa Habari, Vijana na Michezo Emmanuel Nchimbi alisema Taifa litaendelea kukumbuka mchango wa Dr. Remmy hasa kwa kuwa mkongo wa kwanza kupigania sanaa ya Tanzania miaka mingi iliyopita.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.